Tuesday, July 13, 2010

wageni wafunika mazoezini

Kutoka mazoezini leo, tovuti imegundua kuwa wachezaji wapya waliojiunga na timu ya Azam FC wanafanya vizuri hali iliyompa matumaini kocha Itamar Amorin.

Azam FC imefanya usajili kwa kuongeza wachezaji wapya ili kuimarisha kikosi hicho ambacho kina malengo ya kuwa nafasi ya juu katika ligi kuu ijayo.

Wachezaji wapya walikuwepo mazoezini leo ni Mrisho Ngassa, Ramadhani Chombo 'Ridondo', Jackson Chove, Mohamed Slum, Kally Ongala na Jabir Aziz.

Wachezaji hao wameonekana wakishirikiana vyema na wachezaji waliokuwepo katika timu hiyo, ushirikiano huo kama utaendelea vizuri, timu itakuwa katika nzuri zaidi.Kutoka mazoezini leo, tovuti imegundua kuwa wachezaji wapya waliojiunga na timu ya Azam FC wanafanya vizuri hali iliyompa matumaini kocha Itamar Amorin.


No comments:

Post a Comment