Tuesday, July 13, 2010

Azam kucheza na Ngorongoro jumamosi


Timu ya Azam siku ya Jumamosi itakuwa ikifanya mechi yake ya mazoezi dhidi ya timu ya taifa ya vijana chini ya miaka ishirini U20, Ngorongoro Heroes, katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Ikiwa ni mechi ya kwanza ya majaribio kwa timu ya Azam FC, itatumia fursa hiyo kuwapa mazoezi Ngorongoro Heroes ambao wapo katika maandalizi ya kucheza mechi yakufuzu kucheza fainali za Afrika kwa vijana dhidi ya Ivory Coast mwishoni mwa mwezi huu.

Kocha Itamar amesema, mechi hiyo itakuwa muhimu pia kwa timu ya Azam ambayo itakuwa ikifanya maandalizi kwa ajili ya safari ya Ufaransa na ligi kuu ijayo.

“Ngorongoro ni timu imara na nzuri, italeta ushindani mkubwa kwa Azam kwani ina majaribio yake ya kwanza kwa yatakayosaidia kujua uwezo wa timu mapema ili kurekebisha sehemu zitakazokuwa na mapungufu.” aliongeza Itamar.

No comments:

Post a Comment