Sunday, June 27, 2010

kumbe Nadir Haroub Canavaro yupo huru

WACHEZAJI Mussa Hassani ‘Mgosi’ wa Simba na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Yanga ni miongoni mwa wachezaji 38

wa Simba na Yanga ambao wapo huru kwa kuwa wamemaliza mikataba yao inayotambuliwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Ofisa Habari wa TFF Florian Kaijage jana alitangaza orodha ya wachezaji 155 wa timu mbalimbali ambao ama wametemwa au wamemaliza mikataba yao katika klabu tisa kati ya 12 zitakazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.

Katika orodha hiyo ya wachezaji waliomaliza mikataba yapo majina ya Mgosi na Haroub, ambapo awali ilinukuliwa na viongozi wa klabu hizo kongwe nchini kuwa wachezaji hao bado wana mikataba halali na klabu hizo, hivyo hawezi kujiunga na klabu nyingine pasipo kufanya mazungumzo.

Mbali na Mgosi na wachezaji wengine waliomaliza mikataba yao kwa Simba ni Ramadhani Chombo na Jabir Aziz ambao tayari wamejiunga na klabu ya Azam, Mohamedi Banka, Salum Kanoni, Juma Jabu, Kelvin Yondani, Juma Nyoso,Nico Nyagawa, David Naftali na Mohamedi Kijuso.

Wengine ni Haruna Shamte, Adam Kingwande, Ulimboka Mwakingwe, Salim Aziz, George Nyanda, Ally Mustapha, Meshack Abel na Deo Munishi.

Kwa upande wa Yanga wachezaji waliomaliza mikataba yao mbali na Cannavaro ni kipa Obren Cuckovic, Shadrack Nsajigwa, Nurdin Bakari, Abdi Kassim, Godfrey Bonny, Bakari Mbegu, Moses Odhiambo, Kabongo Honore, Boniface Ambani, Hamisi Yusuf, Fred Mbuna,Vicent Barnabas na Ally Msigwa.

Klabu ya Yanga imetangaza kuwatema wachezaji wake Amir Maftah na Mcameroun Robert Mba kwa madai ya utovu wa nidhamu ndani ya klabu hiyo.

Mgosi na Cannavaro wamekuwa wakihusishwa kutaka kujiunga na Azam ya Dar es Salaam.

Katika orodha hiyo wachezaji 23 wa Mibwa wamemaliza mikataba yao, ambapo timu nyingine na idadi ya wachezaji waliomaliza mikataba katika mabano ni Majimaji (25),Toto Afica (9), Kagera Sugar (26), Azam (17), JKT Ruvu (9),African Lyon(8).

Kwa upande wa Azam wachezaji wake waliomaliza mkataba na klabu hiyo imetangaza haitaongeza ni Habibu Mhina, Crispine Odula, Maridadi Haule, Nsa Job, Osborne Monday, Said Sued, Salum Machaku, Yahya Tumbo, Ben Kala na Shaaban Kisiga.

Wachezaji waliomaliza mikataba yao na wapo huru ni Vladmir Niyonkuru, Ibrahim Mwaipopo, Ibrahim Shikanda, Dan Wagaluka, Luickson Kakolaki, Erasto Nyoni na Philip Alando.

Ambani amtabiria makubwa Ngasa


MSHAMBULIAJI wa Yanga, Boniface Ambani amewataka wanachama na mashabiki wa timu hiyo kumpa ushirikiano kiungo mshambuliaji wa Azam FC, Mrisho Ngassa kama alivyokuwa akiitumikia klabu yao.

Ambani ambaye yupo nchini Kenya kwa ajili ya mapumziko ameliambia Championi Ijumaa kuwa, Ngassa asionekane kama msaliti baada ya kutimkia Azam, kwa kuwa viongozi wa timu hiyo walishindwa kumtekelezea mahitaji yake.

kwa mujibu wa gazeti la Champion, “Hakuna mchezaji asiyeipenda klabu yake milele, ni vema mashabiki wakatambua hilo, wanaotakiwa kutupiwa lawama ni viongozi ambao kama wangekuwa na nia ya kumhitaji aendelee kuichezea klabu hiyo naamini wangeweza kumbakisha kwa kiasi chochote.

“Pia itambulike soka ni sehemu ya maisha, kipindi ambacho mchezaji anawika ndiyo hicho cha kukitumia kuliko kuendelea kuchezea timu kwa mapenzi siyo kwa ajili ya maisha ya baadaye,” alisema Ambani ambaye naye amekuwa akihusishwa na mipango ya kuhamia Azam.

Katika msimu wa 2008/2009 Ambani alitwaa tuzo ya ufungaji bora, lakini aliiachia tuzo hiyo msimu uliopita na kwenda kwa Mussa Mgosi.

Papic asema TFF ni wavurugaji


KOCHA wa Yanga, Kostadic Papic amepinga kanuni mpya ya usajili iliyotangazwa na Shirikisho la Soka la Tanzania(TFF) la kusajili wachezaji watano wa kigeni kwa kueleza kuwa kanuni hizo zinavuruga taratibu za klabu.

Kauli ya Mserbia huyo imekuja baada ya TFF kusisitiza kuwa klabu za Ligi Kuu sasa zitaruhusiwa kusajili na kuchezesha wachezaji watano wa kigeni tofauti na msimu uliopita ambapo zilisajili kumi.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu kutoka Serbia aliko mapumzikoni, Papic alisema kuwa kitendo cha TFF kutoa sheria ya wachezaji watano wa nje kusajiliwa ni kuzinyima haki klabu ambazo zimekuwa na maandalizi makubwa kwa ajili ya msimu mpya wa ligi na mashindano yanayowakabili.

"Si sahihi kabisa, ligi imeisha tangu mwezi Aprili, kwa nini basi tangu mwezi Machi kabla ya ligi kuisha wangeweka wazi kanuni hiyo ili kila klabu ijue badala ya kusubiri mpaka sasa ndio wanaweka wazi wakati klabu zimeshatumia gharama nyingi kufanya usajili wake,"alisema Papic ambaye anafahamika kama Bill Clinton, raia wa zamani wa Marekani.

Papic ambaye anatarajiwa kurejea nchini Julai 15, siku tatu kabla ya uchaguzi wa Yanga, alisema, "TFF haitendi haki kwa klabu, wachezaji na sisi makocha, hichi kitu wanachokifanya hakuna sehemu yoyote duniani kinafanywa si sahihi na si haki."

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Wiki iliyopita TFF iliweka bayana kuwa utaratibu mpya wa usajili wa kutumia wachezaji watano ni wa kimataifa kwa msimu mpya utakaoanza Agosti 21 badala ya 10 kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Kanuni hiyo mpya ya TFF inatoa ahueni kwa wachezaji wa ndani, lakini ni mwiba mchungu kwa klabu za Yanga na Simba ambazo zimesheheni wachezaji wa kigeni.

Mpaka sasa ina wachezaji wanne ambao ni Yaw Berko, John Njoroge, Wisdom Ndlovu na Robert Jama Mba(ambaye ametimuliwa) na kocha wao Papic anatarajiwa kutua nchini na wachezaji wengine watatu ambao ni Kenneth Asamoah, Ernest Boakye, na Isaac Boakye, raia wa Ghana na kufikisha idadi ya wachezaji saba.

Kufuatia kanuni hiyo Yanga italazimika kuwaacha wachezaji wawili wa kigeni ili kwenda sambamba na kanuni hiyo ya TFF.

Kwa upande wa Simba, inao Joseph Owino, Hillary Echesa, Jerry Santo, Mike Barasa, Emmanuel Okwi na Patrick Ochan ambaye ni kiungo, raia wa Uganda na hivyo kulazimika kumwacha mchezaji mmoja kati ya hao.

England out, waishia kulilia goli laLampard

PAMOJA na kupokea kipigo cha kusikitisha cha mabao 4-1 kutoka kwa Ujerumani, England wamemshutumu mwamuzi Jorge Larrionda wa Uruguay aliyekata bao la kusawazisha wakati shuti la kiungo wao Frank Lampard lilipopiga mwamba wa juu na kuanguakia ndani ya mstali.

Bao hilo lilikataliwa na mwamuzi Jorge Larrionda wa Uruguay ikiwa muda mfupi baada ya England kupata bao la kwanza huku Ujerumani ikiongoza kwa mabao mawili, ambapo hata mwamuzi msaidizi Pablo Fandino hakuona mpira kama ulikuwa umevuka mstali wa goli.

Bao hilo lililokataliwa lilipoonyeshwa kwenye marudio ya televisheni ilionekana mpira huo ulivuka mita moja ya mstali wa goli.

Alikuwa ni Frank Lampard ambaye alipiga shuti hilo akiwa mita 40 ambapo kipa wa Ujerumani, Manuel Neur alishindwa kulizuia.

Bao hilo lililokataliwa linafananishwa na bao la tatu la England ambalo lilifungwa na Geoff Hurst mwaka 1966 katika fainali dhidi ya Ujerumani magharibi wakati huo, ambapo wajerumani wanapinga bao hilo halikuvuka mstali na linajadiliwa mpaka leo,katika mechi hiyo England ilishinda 4-2.

Akilizungumzia bao la jana, mwamuzi wa zamani wa Ujerumani Helmut Krug aliiambia televisheni ya Ujerumani kwa England wamekataliwa bao.

"Hilo ni kosa ambalo haliwezi kusameheka, mwamuzi msaidizi alitakiwa kuona, mpira ule ulivuka mstali, mwamuzi msaidizi alitakiwa kuona bila hata ya kurudia kutazama tukio hilo,"alisema Helmut Krug.

Rais wa Shirikisho la soka la Ujerumani Theo Zwanziger aliongeza kwenye mahojiano na televisheni ya Ujerumani wakati wa mapumziko kwamba mwamuzi alitakiwa kuona mpira umevuka mstali pale pale alipokuwepo.

"Tunatakiwa tusimamie sheria za soka tulizonazo, ninaweza kuona kwamba mashabiki wa soka wa England hawakufurahia maamuzi ya mwamuzi kukataa bao, niliweza kuona mpira ule uliingia golini,"alisema Zwanziger.

Tukio hilo litakuwa limechochea uhasama wa timu hizo pinzani England na Ujerumani, pia linatarajiwa litachochea kuanzisha mjadala kwa FIFA kuanza kutumia teknolojia ya video ili kuweza kuwasaidia waamuzi kutatua kutoa maamuzi katika mazingira magumu.

Katika mchezo huo mshambuliaji chipukizi Thomas Mueller alifunga mabao mawili pekee yake baada ya Miroslav Klose na Lukas Podolski kuifungia Ujerumani mabao mawili Ujerumani.

England ilipata bao lake la kufutia machozi lililofungwa na beki Matthew Upson katika dakika 37 England kabla ya bao la Lampard kukataliwa dakika moja baadaye.

JENGO LAU 11
DAKAR; Watu 11 wamepoteza maisha kaskazini mwaSenegal baada ya jengo walilokuwa wamekaa na kuangalia mechi za Kombe la Dunia kuanguka ghafla katika mji wa Matam uliopo kaskazini mwa Darak.

Tukio hilolilitokea wakati mashabik hao wakishudia mechi kati ya Uruguay dhidi ya Korea Kusini.

APS ilimkariri afisa usalama akisema watu wengine wawili wameumia vibaya baada ya kudondokewa na jengo hilo.

Senegal haijafuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka huu, lakini mashindano hayo yamekuwa yakiwavuta watu wengi na kufutilia kupitia vituo mbalimbali vya televisheni.

Saturday, June 26, 2010

Wanahabari klabuni Azam FC


Wana habari wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Azam FC makao makuu ya Azam FC, hapa ilikuwa siku Azam FC ilipowatambulisha wachezaji wake wapya wa msimu wa 2010/11 makao makuu ya klabu ya Azam FC Mzizima jijini Dar es Salaam

karibu Ngasa

Ngasa kushoto, Mzee Said Mohammed na Jackson Chove, hapa ilikuwa siku ya utambulisho wa wachezaji hawa Azam FC

Azam FC new kit





Azam FC will soon introduce its own jersey and become the first Tanzanian Team to own quality shirts that will also be available for its fans, the jersey will be available in stores across the country,

Ngassa finally lands at Azam


Former Yanga striker Mrisho Ngassa, bought for a record-breaking Sh58m, by Azam FC, was introduced to officials of his new club in Dar es Salaam yesterday.

Ngassa who also turns for the national side, Taifa Stars, was introduced alongside former JKT Ruvu goalie Jackson Chove at a short ceremony held at the team’s headquarters at Pugu Road in Dar es Salaam. By sharp contrast, however, the latter, Taifa Stars’ second goalie, pocketed a merely Sh3million for a two-year stint at the team.

Ngassa has broken the transfer record of custodian Juma Kaseja who crossed over from Simba to Yanga for Sh36 million.

Azam FC vice president Said Mohammed said they had succeeded in recruiting Ngassa after two days’ negotiations with Yanga.

“The money we have spent on recruiting him indicates that he is a good player who will make the team perform well in the league,” he said.

“I am very happy to be here. I should also thank Yanga officials for releasing me to play for Azam. This is what we call greener pastures,” the joyous Ngassa, who was given jersey No. 16, remarked.


Azam FC Uhai Cup 2009


Aliyekuwa nahodha wa Azam FC Academy 2009 Bakari Mlenge akipokea kikombe cha Uhai Cup 2009

Redondo: Nitawaonyesha kazi



REDONDO amesema kuondoka Simba kumemfanya awe huru zaidi na atacheza soka la hali ya juu msimu ujao zaidi ya lile lililoonekana Msimbazi.

Mchezaji huyo aliyemaliza mkataba na Simba amejiunga na Azam kwa mkataba wa miaka miwili lakini akasisitiza kuwa bado mpango wake wa kwenda Al-Hodood ya Misri uko palepale.

"Msimu ujao nitafanya kazi kwa uhuru sana, naamini nitacheza soka sana kuliko nilivyokuwa Simba, haimaanishi kuwa siku huru mwanzoni lakini maisha ya huku yananifanya niongeze nguvu sana,"alisema Redondo ambaye jina lake halisi ni Ramadhani Chombo.

"Nimekutana na changamoto mpya na mategemeo ni makubwa sana hasa kutokana na Azam ilivyo na aina ya wachezaji iliyowasajili, naamini tutacheza mpira sana na mimi nitakuwa mmojawapo.

"Nimesaini mkataba mrefu lakini endapo dili yangu ya Misri ikikaa vizuri nitakwenda nimewaambia viongozi wangu na wamenielewa,"alisisitiza mchezaji huyo aliyewahi kuchezea Ashanti United iliyoshuka daraja.