Thursday, July 29, 2010

Azam FC JKT Ruvu Ruvu sare ya 1-1, kucheza na Simba usiku kesho Amaan Stadium





Zikicheza soka la kuvutia wakati wote wa mchezo, timu za Azam FC na JKT Ruvu zimetoshana nguvu kwa kufungana goli 1-1 katika mchezo wa kuvutia wa kirafiki uliochezwa kwenye dimba lililokarabatiwa wa Amaan visiwani Zanzibar.

Azam FC ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata goli katika dakika ya 25 lililofungwa na Ibrahim Mwaipopo kwa njia ya penati baada ya beki wa JKT Ruvu Stephano Nkomola kuunawa mpira katika eneo la hatari

Bao la JKT Ruvu lilifungwa katika dakika ya 85 baada ya mchezaji mpya wa JKT Ruvu Pius Kisambale kuukwamisha wavuni mpira wa krosi toka wingi wa kulia.

Katika mchezo wa leo, mchezaji Kalimangonga Ongala ambaye aliingia kipindi cha pili alikonga nyoyo za mashabiki kutokana na kuonesha soka la hali ya juu. Kaly alikuwa fundi sana wa kuuficha mpira, alikuwa na nguvu sana za kupambana lakini zaidi ya yote alikuwa na spidi ya kutosha na ameonesha matumaini makubwa sana.

Mchezaji Mrisho Ngasa kama kawaida yake aling’ara sana uwanjani akicheza kwa kiwango chake cha siku zote. Licha ya kupoteza nafasi mbili tatu za kufunga Ngasa alikuwa hatari muda wote wa mchezo.

Ibrahim Mwaipopo ambaye ameonekana kuongezeka misuli na spidi leo amecheza soka la hali ya juu sana, mwaipopo ana sifa iliyojificha nayo ni uwezo wa kuutuma mpira umbali mrefu na mpira ukafika pahala alipokusudia, leo ndicho kitu alichukuwa akikifanya Ibrahim, alikuwa akipiga pasi ndefu kulia na kushoto na zilikuwa zikifika barabara, penati yake aliifunga kwa ufundi mkubwa sana ambapo mpira ulianza kugonga mwamba wa juu kabla ya kutinga nyavuni. inaonekana kama licha ya kuja nyota kibao wa sehemu ya kiungo lakini nyota huyo wa Tanzania anaelekea kuilinda nafasi yake vizuri.

Tuseme nini kuhusu Jabir Aziz? Kama kuna mchezaji ambaye Azam FC imelamba dume kwenye usajili basi ni chipukizi huyu. Kwa wanaofuatilia soka la kimataifa na wanaomjua vizuri Xavi Harnandes wa FC Barcelona basi kwa huku bongo jabir ni photocopy na Xavi, Jabir leo alikuwa kila sehemu uwanjani akimiliki mipira na kuisambaza kwa wahusika utadhani mashine. Ama hakika atakaporudi Salum Abubakar toka timu ya Taifa ya Vijana Azam FC itatisha sehemu ya katikati.

Leo kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha Azam FC tumeshuhudia mapacha wawili sehemu ya ulinzi, Ibrahim shikanda upande wa kulia na Patrick Mafisango upande wa kushoto. Nawaita mapacha kutokana na aina ya uchezaji wau kwa lugha ya kiingereza ningeweza kuwaita stylish players. Kama ilivyo Shikanda, Mafisango alikuwa akicheza kwa nidhamu na ufundi mkubwa sana, anakaba kwa kutumia akili sana, anaelekeza wenzake nini cha kufanya, ana mbinu na ujuzi wa kuwasoma wapinzani kwa haraka lakini zaidi ya yote ana kipaji cha kumiliki mpira na hawa ni wachezaji ambao hawakupoteza pasi leo uwanjani.



John Bocco Adebayor leo alikuwa burudani…. Alikuwa akimiliki mipira vizuri na kuigawa kwa wenzake lakini pia wakati alipotakiwa kupiga alipiga na kulenga goli vizuri. Bocco ambeye ndiye mfungaji bora wa Azam FC wa wakati wote akiwa na miaka 20 tuu ameonesha kuwa mazuri mengi bado hayajaiva na yanaendelea kuja toka kwa kijana huyu mrefu mwenye uwezo wa kupiga kwa miguu yote na kichwa.

Aggrey Morris na Eraso Nyoni wameonesha kuwa wao ndiyo pacha bora ya Azam FC kwa upande wa walinzi wa katikati. Aggrey ana Nguvu nyingi sana na Erasto ana akili nyingi sana. Mchanganyiko huu ni mzuri sana kwenye timu na ndicho walichokionesha uwanjani, walikuwa wakipeana majukumu vizuri sana na inaonekana kwamba msimu huu tutakuwa na kikosi bora kabisa.

Mechi nyingine ni keshokutwa ambapo Azam FC itacheza usiku na Simba SC

Wednesday, July 21, 2010

Azam fc yaibanjua Ruvu Shooting






Baada ya kutoa sare na Ngorongoro Heroes, Azam FC leo imepata ushindi wa 2-1 dhidi ya timu ya Ruvu Shooting katika uwanja wa Ruvu Mkoani Pwani.

Azam FC ilianza kupata goli la kwanza dakika ya 15 ya mchezo lililofungwa na mchezaji John Bocco baada ya kuunganisha krosi ya Faraji Hussein.

Goli hilo lilidumu kwa dakika 20, baada ya beki wa kutumainiwa wa Azam FC, Aggrey Morice kuandika goli la pili kwa mpira wa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa adhabu ndogo uliyopigwa kiufundi na Ibrahim Mwaipopo.

JKT walipata penati katika dakika za mwisho kipindi cha kwanza lakini golikipa mpya wa Azam Jackson Chove aliokoa

Matokeo hayo yalizipeleka timu zote mbili mapumziko, huku Azam FC ikiongoza kwa 2-0.

Kipindi cha pili tiu Azam FC ilifanya mabadiliko kuimarisha ngome yake kwa kumtoa Erasto Nyoni na Seleman Kassim ‘Selembe’ na nafasi zao zikachukuliwa na Salum Swed na Jamal Mnyate.

Dakika ya 51 Ruvu Shooting walipata goli kupitia kwa mchezaji Salum Kimai baada ya kuachia shuti lililotinga wavuni na kumuacha kipa wa Azam FC, Jackson Chove akishangaa.

Goli hilo lilileta mabadiliko ya mchezo kwani timu zote zilicheza kwa kukamiana huku Ruvu Shooting wakitaka ushindi katika mechi yao ya nyumbani, na Azam wakiitaji kulinda lango wasipoteze mechi ya leo.

Katika mechi hiyo ya kirafiki, golikipa Jackson Chove alipewa kadi nyekundu baada ya kumkanyaga mchezaji Paul Ndauka na mchezaji wa Ruvu Shooting Gido Chawala alipewa kadi nyekundu baada ya kumsukuma Chove baada ya kumfanyia madhambi Ndauka.

Kocha wa Azam FC,Itamar Amorin amesema kikosi chake kimebadilikana kuimarika kuliko walipokuwa wakicheza mechi yao ya kwanza.

“Timu imecheza vizuri, kuna mabadiliko makubwa hasa upande wa pasi, ball position na ball control ukilinganisha na mechi iliyopita, kwani wameimarika zaidi.” Alisema Itamar.

Ameongeza amerekebisha makosa yaliyotokea katika mechi dhidi ya Ngorongoro, na kuifanya timu hiyo kuwa katika hali nzuri zaidi.

Akizungumzia uwanja wa Ruvu, Itamar alisema ni uwanja mzuri, una nyasi nzuri lakini zimezidi sana na hazifai kwa kuchezea mpira kwani mpira unakwama mara na kupoteza pasi za wachezaji.

Azam FC, Jackson Chove/David Mwasongwe, Ibrahim Shikanda/Malika Ndeule, Mau Bofu, Agrey Morice, Erasto Nyoni/Jamal Mnyate, Ibrahim Mwaipopo, Faraji Hussein/Ally Mkuba, Ramadhani Chombo ‘Ridondo’, John Bocco/Ally Manzi, Mrisho Ngassa/Cosmas Lewis, Seleman Kassim/ Jamal Mnyate.

Yonatus Mbalimo, Mangasin Mbomus, Peter Moses, George Akitenda, George Osey, Owen Mikumba, Godo Chawala, Faraji Makumbo, Martin Lupati, Salum Chimai, Revocatus Maliwa.

Thursday, July 15, 2010

Mambo ya Chamazi












Picha hizi zinaonesha maendeleo ya ujenzi wa kituo cha michezo cha Azam FC ambapo kwa mujibu wa Ramani ya Ujenzi kutakuwa na Bwawa la kuogelea la kiwango cha Olympic, hostels za wachezaji, kiwanja cha mazoezi cha nyasi bandia kama kile cha Karume, kiwanja cha mazoezi kingine cha nyasi za kawaida kama za uwanja mpya wa Taifa na uwanja mkubwa wa michezo.

Ujenzi wa kituo hiki unafanywa kwa Awamu ambapo awamu ya kwanza inahusisha hostels za wachezaji, kiwanja cha mazoezi cha nyasi bandia, bwawa la kuogelea, kanteen ya chakula na Uzio wa eneo lote.



Azam Kuwa na Uwanja wake

Habari kwa hisani ya gazeti na Mwananchi

KLABU ya Azam imetangaza kikosi chake na kuweka bayana ujenzi wa uwanja wao kisasa huko Chamanzi Jijini Dar es Salaam na kuhaidi kuanza kutumia kwenye michezo yake ya Ligi Kuu katika mzunguko wa pili.

Klabu hiyo itakuwa ya kwanza hapa nchini kujenga uwanja wa kisasa ambao utakuwa ukitumika kwenye michezo ya Ligi Kuu.

Mwenyekiti wa Azam, Said Mohamed alisema kuwa tayari wameshaingia mkataba na kampuni moja iliyopo Afrika Kusini kwa ajili ya kujenga uwanja huo kwa kutumia nyasi za bandia.

Alisema mbali na nyasi hizo wameshaanza ujenzi wa hosteli za wachezaji wao ambazo zitatumika kama kambi ya wachezaji na zitaanza kutumika rasmi mzunguko wa pili ya Ligi Kuu Tanzania bara unaoanza Agosti 21.

Pia, kambi hiyo itakuwa na kila kitu ambacho ikiwemo sehemu ya kufanyia mazoezi ya viungo ( GYM) ambayo itatumika kwa wachezaji wao kufanya mazoezi ya viungo.

Kwa upande wa wachezaji wanaowaacha mwenyekiti huyo alisema kuwa timu yao imesajili 22 na vijana chini ya miaka 20 sita.

Wachezaji walioacha ni Chrispine Wadenya, Hadid Mhana, Maridad Haule, Nsa job, Said Swed, Salum Machaku, Yahaya Tumba, Ben Kalama, Shaban Kisiga na Dan Wagaluka.

Waliowasajili wapya kwa ajili ya msimu ujao ni Mohamed Binslum, Jackson Chove, Jabil Azizi, Mrisho Ngassa, Kali Ongala ( GIF Sweden) Mutesa Patrick (APR Rwanda) na Ssenyonjo Peter (Polisi Uganda).

Kocha wa timu hiyo Amorian Itamaa alisema kuwa kuacha kwa wachezaji hao wameangalia vitu vingi ikiwemo nidhamu na kushuka kwa uwezo wake uwanjani.

Alisema kunabaadhi ya wachezaji wamekuwa na nidhamu mbaya katuika kambi na mazoezini na wengine wameshuka uwezo ndio maana tumewaacha katika usajili wetu mpya.

Aidha alisema kuwa mchezaji yoyote yule hawe na jina hasiwe na jina kama hatakuwa na midhamu mbaya atawajibishwa kwani msimu huu wamejipanga kuchukua ubingwa wa ligi kuu.

Hata hivyo wachezaji wote waliosajiliwa na klabu hiyo wameingia kambini katika ufukwe wa Bamba beach uliopo Kigamboni nje kidogo ya Dar es Salaam.