Tuesday, July 13, 2010

Azam yatangaza usajili 2010, yamtwaa rasmi Patrick mafisango, Ngasa haendi kokote




ikiwa imesalia siku moja kufikia mwisho wa usajili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu utakaoanza August mwaka huu, uongozi wa Azam FC umetangaza kukamisha usajili wake na kuanza kwa maandalizi kwa ajili ya ligi hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa Azam FC, Said Mohamed amesema usajili wa mwaka huu wameacha wachezaji kumi waliokuwepo msimu ulipita na kubakisha wachezaji 14, huku wakisajili wachezaji wapya nane na kupandisha jumla ya wachezaji sita kutoka katika timu ya vijana 'Azam Academy'.

“Katika usajili wetu tumesajili wachezaji watatu kutoka nje ya Tanzania na watano kutoka katika vilabu vya hapa nchini, tumezingatia taratibu za TFF kwa kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi watano, ni matumaini yetu wachezaji wetu watafanya vizuri” alisema Mohamed.

Mohamed aliongeza kuwa Azam itakuwa na jumla ya wachezaji watano wa kigeni baada ya kuongeza wachezaji watatu ambao wataungana na wengine wawili walipo katika timu hiyo.

Uongozi umewataja wachezaji wapya waliosajiliwa na timu hiyo kuwa ni Mohamed Binslum (Huru) Jackson Chove(JKT Ruvu), Jabir Aziz na Ramadhan Chombo 'Redondo' (Simba), Mrisho Ngassa (Yanga), Kalimangonga Sam Daniel Ongala Rampling 'Kali Ongala' (GIF-Sweeden), Patrick Mutesa Mafisango (APR- Rwanda) na Peter Senyonjo (Polisi-Uganda.)

Wachezaji waliobaki ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jamal Mnyate, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Vladmir Niyonkuru, Philip Alando, Luckson Kakolaki, Malika Ndeule, Aggrey Morice, Salum Swed, Ibrahim Shikanda, Ally Manzi, Seleman Kasim 'Selembe' na Ibrahim Mwaipopo.

Makamu Mwenyekiti aliongeza kuwa timu hiyo haikuwaacha mbali wachezaji wao wa timu ya vijana 'Azam Academy', imepandisha wachezaji sita ambao ni Sino Augustino, Himid Mao, Mau Ali, Tumba Swed, Ali Mkuba na Samih Nuhu.

Mohamed aliwataja wachezaji walioachwa kuwa ni Chrispin Odula, Habib Mhina, Maridad Haule, Nsa Job, Said Swed, Salum Machaku, Yahya Tumbo, Ben Kalama, Shaaban Kisiga na Dan Wagaluka.

Azam kambini Bamba beach Kigamboni.

Timu ya Azam FC kesho inataraji kuweka kambi Bambabay maeneo ya Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya maandalizi ya ligi kuu.

Azam FC ikiwa kambini itakuwa ikifanya mazoezi mara mbili kwa siku, asubuhi itakuwa ikitumia uwanja wa Uhuru na jioni kufanya mazoezi katika viwanja vilivyopo Kigamboni.

“Tumeamua kwenda Kigamboni kutokana na kupata eneo zuri kwa ajili ya kambi, pia kuna viwanja vizuri vya kufanyia mazoezi” alisema mwenyekiti wa Azam FC, Said Mohamed.

Aliongeza kuwa timu itakuwa huko kwa muda maalum huku ikisubiri taarifa maalum kutoka TFF kama kutakuwa na safari ya kwenda ufaransa, kama haitakuwepo timu itaenda Zanzibar kwa ajili ya maandalizi

Wachezaji wapya

Mohamed Binslum (Huru)

Jackson Chove(JKT Ruvu)

Jabir Aziz na Ramadhan Chombo 'Redondo' (Simba)

Mrisho Ngassa (Yanga)

Kalimangonga Sam Daniel Ongala Rampling 'Kali Ongala' (GIF-Sweeden),

Mutesa Mafisango (APR- Rwanda

Peter Senyonjo (Polisi-Uganda.)

Wachezaji waliobaki

John Bocco,

Erasto Nyoni

Jamal Mnyate

Salum Aboubakar 'Sure Boy'

Vladmir Niyonkuru

Philip Alando

Luckson Kakolaki

Malika Ndeule

Aggrey Morice

Salum Swed

Ibrahim Shikanda

Ally Manzi

Seleman Kasim 'Selembe'

Ibrahim Mwaipopo

Waliopandishwa Kutoka Azam Academy

Sino Augustino

Himid Mao

Mau Ali

Tumba Swed

Ali Mkuba

Samih Nuhu

walioachwa

Chrispin Odula

Habib Mhina

Maridad Haule

Nsa Job

Said Swed

Salum Machaku

Yahya Tumbo

Ben Kalama

Shaaban Kisiga

No comments:

Post a Comment