Tuesday, July 13, 2010

Msimu mpya jezi mpya


Msimu mpya na mambo mapya, Azam FC wameanza mazoezi wakiwa na jezi mpya tofauti na zile walizokuwa wakizitumia msimu ulipoita.

Azam ya sasa ikiwa mazoezini inavaa jezi zenye rangi ya bluu iloyoiva yenye rangi ya chungwa mabegani, huku wakitumia kaptura nyeusi zilizo na mchirizi wa rangi ya chungwa, namba za wachezaji na maandishi ya Azam yanarangi ya chungwa.

Makocha msimu huu wanavaa jezi nyeupe zenye mistari miwili ya rangi za blu pembeni, huku kaptura zao zikiwa nyeupe na mistari miwili ya rangi za blu, jezi hizo zina maandishi yenye rangi za chungwa.

Msimu uliopita Azam FC walikuwa wakitumia jezi zilizokuwa katika mfumo wa Tshirt zenye rangi ya chungwa, na makocha walikuwa wakivaa jezi za rangi nyeupe na bluu bahari.

No comments:

Post a Comment